Hosea 14

Toba Iletayo Baraka


1 aRudi, ee Israeli, kwa Bwana Mwenyezi Mungu wako.
Dhambi zako zimekuwa
ndilo anguko lako!

2 bChukueni maneno pamoja nanyi,
mkamrudie Bwana.
Mwambieni:
“Samehe dhambi zetu zote
na utupokee kwa neema,
ili tuweze kutoa matunda yetu
kama sadaka za mafahali.

3 cAshuru hawezi kutuokoa,
hatutapanda farasi wa vita.
Kamwe hatutasema tena ‘Miungu yetu’
kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza,
kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”


4 d“Nitaponya ukaidi wao
na kuwapenda kwa hiari yangu,
kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.

5 eNitakuwa kama umande kwa Israeli;
atachanua kama yungiyungi.
Kama mwerezi wa Lebanoni
atashusha mizizi yake chini;

6 fmatawi yake yatatanda.
Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni,
harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.

7 gWatu wataishi tena kwenye kivuli chake.
Atastawi kama nafaka.
Atachanua kama mzabibu,
nao umaarufu wake utakuwa
kama divai itokayo Lebanoni.

8 hEe Efraimu, utasema, ‘Mimi nina shughuli gani tena na sanamu?’
Nitamjibu na kumtunza.
Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi;
kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”


9 iNi nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya.
Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa.
Njia za Bwana ni adili;
wenye haki huenda katika njia hizo,
lakini waasi watajikwaa ndani yake.
Copyright information for SwhKC